Abdukiba: Ali Kiba Amenitengenezea Njia

Mwanamuziki wa Bongo fleva Abdu Kiba ambaye ni kaka wa Supastaa wa Bongo fleva, Ali Kiba amefunguka na kudai kuwa kaka yake ameshiriki katika kumtengenezea njia kwenye sanaa.

Ali Kiba alianza kufanya muziki miaka ya nyuma sana ni moja kati ya msanii mkongwe ambaye amedumu kwenye gemu mpaka leo bila kuchuja tofauti na wasanii wengine wengi waliopotea.

download latest music    

Abdu Kiba ameibuka na kukanusha maneno yanayoongelewa na watu wanaodai kuwa alikuwa kimya kwa muda mrefu sana kwa sababu kaka yake Ali Kiba alikuwa anamkataza kufanya mziki.

Kwenye mahohiano aliyofanya na Enews ya East Africa Tv, Abdu Kiba amedai kuwa Ali Kiba alikuwa akimtengenezea njia nzuri ya kuja kufanya mziki mzuri na ni mtu anayetakiwa kusikilizwa sana kwenye game:

Kiukweli kwanza nimshukuru Mungu kwa ukimya wote niliokaa na mpaka nimerudi mafans wamenipikea alafu tena naamini mziki Una changamoto tukisikiliza maneno ya watu wanayozungumza pembeni ni changamoto ambazo mimi napata na ndizo zilizonikuza kwenye huu mziki hivyo Alikiba na management ilivyoniambia nikae nitulie nisubiri hata mwaka ili nijipange sana ili nikirudi mambo yawe mazuri kama mnavyoona nashukuru Ali Kiba amenitengenezea njia ya kupita”.

Baada ya Abdu Kiba kukaa kimya kwa muda mrefu bila ya kutoa ngoma yoyote maneno Mengi yalizuka huku wait wengi wakidai kuwa Alikiba amemkataza kutoa ngoma lakini hivi karibuni ametoa nyimbo mpya inayoitwa Single aliyomshirikisha Alikiba ambayo inaendelea kufanya vizuri kwenye chati.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.