Aby dady afunguka kuhusu kolabo ya Alikiba na Patoranking kuvuja.

kumekuwepo na  stori mitandaoni kuhusu kuvuja kwa kolabo kati ya msanii wa bongo fleva Alikiba na msanii mkubwa kutoka Nigeria  patoranking, wimbo ambao bado ulikuwa haujatoka rasmi lakini ulishaanza kusikika kwa baadhi ya mashabiki. akiongea  katika kipindi  cha eNews cha EATV producer wa ngoma hiyo anasema kuwa yeye hajui chochote kuhusu kuvuja kwa  wimbo huo, producer huyo anasema kuwa yeye ni mfanya biashara hivyo kuvujisha wimbo huo bila ruhusa ya msanii ni kujikosesha mapato ya kazi yake, hata hivyo anasema bado kulikuwa kuna vitu bado havijakamilika kati yake na msanii huyo ndo maana colabo hiyo haukuwa imeachiwa.

Hata hivyo ikimbukwe kuwa ni kama wiki moja to imepita tangu colabo nyingine kati ya  msanii huyo wa Nigeria ,Patoranking   na msanii mkubwa wa bongo fleva nchini Diamond platinumz kuachiwa na umekuwa ukihit sehemu mbalimbali.

download latest music    

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.