Afande Sele Aukacha Upinzani na Kujiunga na CCM

Mwanamuziki mkongwe na rapa wa muziki wa Bongo fleva Afande Sele ajivua rasmi upinzani siku ya leo na kuhamia chama tawala Chama cha Mapinduzi (CCM).

Afande Sele amejiunga rasmi leo na CCM mbele ya mwenyekiti wa Chama hicho na Raisi wa Jamhuri ya Tanzania John Pombe Magufuli leo Machi 15, 2017.

download latest music    

Afande Sele amefunguka na kudai kuwa sababu kubwa iliyompelekea  kuhamia Chama tawala ni kuunga mkono juhudi za Rais Magufuli katika kupambana na rushwa na kuwajali wanyonge.

Lakini pia Afande Sele amewaomba wanachama wa Chama hiko kumpokea kwa mikono miwili na kumuonyesha ushirikiano katika kujenga nchi yetu na kuonyesha sapoti kwa raisi na serikali kwa ujumla.

Afande Sele kabla ya kujiunga na CCM alishawahi kuwa mwanachama wa CHADEMA na Chama cha ACT Wazalendo ambapo mwaka 2015 alitangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Morogoro Mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.