Afande Sele Awapa Makavu Wanaume Vibenteni

Mwanamuziki Mkongwe wa muziki wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kurap Afande Sele amewatolea uvivu wanaume wote wanaopenda kulelewa na wanawake.

Vijana wa kiume wamekuwa na mtindo wa kutafuta wanawake waliwazidi umri na kulelewa kwa majina wanaitwa Marioo au Vibenteni.

download latest music    

Afande Sele amewatolea uvivu wanaume hao na kudai wanaume wote wanaopenda kulelewa wanaishia kupoteza nguvu zao za kiume.

Tabia ya vijana kupenda kulelewa inawanyima uhuru binafsi, uwezo wa kufikiria unapungua kwa sababu unajikuta muda mwingi unawaza kumfurahisha mtu mwingine na ndio maaan unaweza kukuta hata kufanya mapenzi hujisikii na Kitendo hiko kinasababisha kwa asilimia kubwa kwa kukosa nguvu za kiume na matokeo yake inapelekea kununua dawa za kuongeza nguvu za kiume”.

Kwa sasa imekuwa jambo la kawaida hasa kwa hapa mjini vijana masharobaro wasiopenda kufanya kazi huamua kujitafutia mashuga mama wa kuweza kuwapa huduma mbali mbali.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.