Agnes Masogange Ahukumiwa Kwenda Jela Kwa Miaka 2

Muigizaji wa Bongo movie Agnes Gerald maarufu kama Masogange amekutwa na hatia na mahakama ya hakimu mkazi Kisutu na kuhukumiwa miaka miwili jela au kulipa faini ya shilingi milioni 1.5.

Agnes alifunguliwa kesi na Jamhuri mapema mwaka Jana baada ya kukamatwa nna kutumia madawa ya kulevya aina ya Heroin na ya pili ni kutumia madawa ya kulevya aina ya Oxazepam.

download latest music    

Hakimu wa mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, Wilbard Mashauri ametoa hukumu hiyi Leo na kuieleza mahakama kuwa amekutwa na hatia katika makosa yote mawili.

Hivyo katika kosa la kwanza mahakama inamuhuqkumu kwenda jela kwa miaka miwili au kulipa faini ya shilingi milioni moja na kosa la pili amehukumiwa kwenda jela miezi kumi na mbili au kulipa faini ya shilingi laki tano”.

February 17 mwaka Jana Masogange alitiwa hatiani kwa tuhuma za kutumia madawa ya kulevya ambapo alienda kupimwa na mkemia mkuu Wa serikali.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.