Agnes Masogange Alikuwa Mtu Wa Watu- Young Dee

Staa wa Bongo fleva David Genzi maarufu kama Young Dee amefunguka na kusema kuwa marehemu Agnes Gerald ‘Masogange’ alikuwa mtu wa watu sana.

Ikiwa imepita wiki moja sasa tangu Masogange aage dunia mastaa wenzake bado wanaendelea kumkumbuka na kumlilia huku ikionekana wazi kabisa kuwa itakuwa ngumu kuziba pengo lake.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Championi Jumatano, Young Dee alisema kipindi cha uhai wake, Masogange alikuwa ni mtu wa watu ambaye alikuwa hapendi ugomvi na hajawahi kusikia akigombana na mtu japo yeye hajawahi kufanya naye kazi.

Japo sijawahi kufanya naye kazi, lakini alikuwa mtu wa watu kwani sijawahi kusikia akigombana na mtu yeyote, kwa sasa wasanii tuendelee kumuomba Mungu na tuachane na maovu pia tuwe wamoja kwani hujui lini utakufa“.

Masogange alifariki dunia Ijumaa iliyopita kwenye Hospitali ya Mama Ngoma iliyopo Mwenge jijini Dar es Salaam baada ya kuugua Ugonjwa wa Nimonia na upungufu wa damu mwilini na kisha kuzikwa wiki hii siku ya Jumatatu kijijini kwao Mbeya.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.