Agness Aliniambia Ana Mchumba Amwemwambia Atulie:-Kajala
Kuna kuwa na stori nyingi sana hasa mtu maarufu anapofariki kwa sababu kila mmoja anataka kuongea kile alichowahi kushare na marehemu, moja ya watu waliofunguka na kuguswa na msiba huu ni msanii wa bongo movies ni kajala ambae anasema kuwa pamoja na kwamba Aggy alikuwa kama alivyo lakini hakuwahi kulinga na mtu.
Kajala anasema kuwa mara ya mwisho kuongea na aggy ilikuwa ni mwezi watatu na walikuwa waitaniana mambo mengi sana
” ni mtu ambae alikuwa unaweza kutaniana nae na kuongea na mtu yoyote yule, alikuwa hana majivuni pamoja na kwamba alikuwa vile alivyo. mara ya mwisho kuchart na aggy ilikuwa mwezi wa tatu nakumbuka na alinitania kuwa sasa hivi nimenenepa sana nikamwambia sawa lakini mbona siku hizi huonekani , akanijibu kuwa sasa hivi ametulia amepata mchumba amemuomba atulie.