Aikah Afunguka Mpango Wa Kuzaa Mtoto Mwingine

Msanii wa Bongo fleva kutoka katika kundi la Navy Kenzo Aikah Mareale amefunguka na kuweka wazi mipango yake ya kuzaa mtoto mwingine na mpenzi wake Nahreel.

Aikah alijifungua mtoto wake wa kwanza anayeitwa Gold Navykenzo mapema mwaka huu na mpenzi wake wa siku nyingi Emmanuel Mkono maarufu kama Nahreel.

download latest music    

Lakini Gold akiwa na Miezi michache tu Aikah amefunguka na kusema yupo mbioni kutaka kuongeza mtoto mwa pili.

Kwenye mahojiano na Risasi Vibes, Aika amesema kuwa tangu amezaa mtoto mmoja ameona raha kuwa mama hivyo basi hana muda wa kujishauri tena bali ni kumleta mdogo wa Gold, mapema wala hana muda wa kupoteza.

Najisikia furaha sana kuwa mama hata wa watoto watano hivi nimeona raha ya kuzaa na hivi sasa niko njiani kuleta mtoto mwingine mambo ya kupishana muda mrefu sio sawa kabisa”.

Aikah na Nahreel wamekuwa Kwenye Mahusiano kwa miaka zaidi ya kumi Lakini hivi karibuni walisema hawana haraka ya kufunga ndoa kwani kuwa na bond ni muhimu zaidi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.