Aikah Afungukia Miaka 10 Ya Mahusiano na Nahreel

Msanii kutoka kundi la Navy Kenzo, Aikah Mareale amefungukia na kuongelea Mahusiano Yake yaliyodumu kwa miaka 10 na mpenzi wake Msanii na mtayarishaji wa muziki Nahreel.

Wiki iliyopita Nahreel na Aikah walisheherekea miaka kumi ya kuwa pamoja tangu walipokutana kwa mara ya kwanza nchini India walipokuwa kimasomo.

download latest music    

Kwenye mahojiano yake na Global Publishers , Aika alifunguka kwamba ndani ya miaka hiyo waliyoishi pamoja kama marafiki wakubwa, wapenzi na watu wanaosi-kilizana, imeweza kuwafundisha vitu vingi kwa sababu wamepitia changamoto nyingi hadi kufika hapo.

Ulishawahi kukaa na mtu miaka 10, lakini unaona ni kama jana tu? Hii ni kutokana na jinsi mlivyoishi katika upendo na urafiki mkubwa, ndivyo tulivyo mimi na Nahreel na tunaunganishwa zaidi na mtoto wetu, Gold“.

Pamoja na kwamba Aikah na Nahreel wamezaa mtoto mmoja anayeitwa Gold lakini wameweka wazi hawana papara ya kuoana kwa sasa endapo muda Ukiwa tayari watafunga ndoa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.