Aikah Navykenzo Afungukia Ndoa na Nahreel

Mastaa wa muziki wa Bongo fleva kutokea katika kundi la Navy kenzo Aikah Marealle amefunguka na kuweka wazi kuwa yeye na mpenzi wake Emmanuel Mkono ‘Nahreel’ wana mipango ya ndoa.

Wasanii hao ambao wamekuwa Kwenye Mahusiano kwa zaidi ya miaka 10 walibahatika kupata mtoto wao wa kwanza mapema mwaka huu anayeitwa Gold Navykenzo.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Global Publishers, Aikah amefunguka na kuweka wazi kuwa pamoja na kwamba wameshazaa nje ya ndoa lakini anaona ni jambo la kawaida na wana mipango ya ndoa.

Kwangu ninaona ni kawaida. Sisi siyo watu wa kwanza kupata nje ya ndoa mtoto, lakini mipango ya kufunga ndoa ipo na muda ukifika tutafunga ndoa.

Lakini pia Aikah ameanika changamoto wanazopitia katika kulea mtoto wao na kufanya muzikI katika wakati mmoja:

Kuna changamoto sana na si jambo rahisi hata kidogo kulea mtoto na kufanya muziki. Tangu tupate mtoto mambo mengi yamekwama kiasi kwamba kuna ‘interview’ nyingi tumezipiga chini ili tu kudili na mtoto. Unajua sisi ni wazazi wapya kwa hiyo mambo mengi tunajifunza“.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.