“Akumbuke alianzia chini mpaka kufika alipo sasa” Harmorapa amjibu Afande Sele

Image: Harmorapa

Kwa sasa hakuna mtu ambaye hamjui Harmorapa kutoka Tanzania. Rapa huyu amekuwa kwenye mitandao kadhaa na wengi hupenda kuongelea nyimbo zake lakini Afande Sele hivi karibuni alidai kuwa hakuwa anamjua Harmorapa hadi liletokeo la Nape kushikiwa Bastola.

Afande Sele
Afande Sele

Maneno haya yanaonekana kuwa yalimuudhi muimbaji huyu ambaye amefunguka kupitia mahojiano yake na EATV. Harmorapa alisema kuwa yeye hana maneno mengi ya kusema lakini kwa sasa Afande Sele anapaswa kujua kuwa hakuna mtu anayeanzia juu kwani pia yeye alianzia chini ndipo afike alipo sasa.

download latest music    

“Niseme tuu yeye kwanza mwenyewe akae chini na kujua na kukumbuka kuwa alianzia chini mpaka kufika level fulani watu wakamkubali.”

Aliendelea kusema,

“Ajue mimi kama Harmorapa sina maneno mengi ila kazi zangu ndiyo zitakuja kumuelekeza kuwa Harmorapa uliyekuwa unamuongelea ndiyo huyu kupitia kazi yangu ndiyo itakuwa imemnyoosha au vipi? na ku’prove ukali wa Harmorapa.”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua