Ali Kiba afunguka kuhusu mipango aliyonayo na lebo yake

Watu wengi ata hawajui kama Ali Kiba ako na lebo yake. Staa huyo ako na wasanii ambao amewasaini kwa lebo yake ambayo sio maarufu.

Wasafi inayomilikiwa na Diamond ndo lebo ambayo inajulikana sana Tanzania na ata nje ya nchi hii. La kushangaza ni kuwa Ali Kiba anamiliki lebo yake.

download latest music    

Akiongea na Mzazi Willy Tuva katika kipindi cha Mambo Mseto ya Citizen Radio, Ali Kiba alifunguka kuhusu lebo yake na mipango yake kuhusu lebo hio.

“Mimi nilisha kuwa na lebo muda mrefu sana, sema kazi zangu hazikuwa za matangazo kama hivyo. Ni muda mrefu nimeanza kufanya muziki na kusaidia watu sio leo, toka nipo katika game kabla sijapumzika nilikuwa na lebo yangu ya muziki lakini haikuwa inatangazwa. Sasa hivi kila kitu kipo kwenye utandawazi, kila mtu anatakiwa kujua Alikiba ana lebo na anafanya hivi na hivi.

“Nipo na wasanii ambao nimewasaini lakini bado sija watangaza wala kutoa kazi zao, tupo kwenye procsess za mwisho kwa sababu kila mtu kasharekodi nyimbo yake bado kushoot video ndio tuwatangazie watu,” Ali Kiba alifunguka baada ya kuulizwa kama angefungua lebo kama baadhi ya wasanii wengine wakubwa.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere