Ali Kiba akiri kuwa Barakah The Prince ako na akili za kitoto

Wambeya wanasema kuwa urafiki baina ya Ali Kiba na Barakah The Prince unadidimia kwasababu ya bifu kati ya Baraka na Ommy Dimpoz.

Inasemekana kuwa ukaribu wa Dimpoz na Ali Kiba umechangia kuzorota kwa urafiki baina ya Kiba na Baraka kwasababu Dimpoz na Baraka hawali sahani moja kwa sasa.

download latest music    
Barakah The Prince na Ali Kiba

Akiongea na kipindi cha XXL cha Clouds FM, Ali Kiba alikiri kuwa Barakah The Prince ako na akili za kitoto ndio maana kuna maadhi ya mambo yanaibuka kwamba haelewani na baadhi ya wasanii wenzake.

“Mimi nadhani ni utoto tu, nadhani ni umri tu lakini Baraka yupo vizuri, ni mtu anayesikiliza na ana rekebishika. Muda mwingine labda umri ndio unampeleka lakini muda mwingine mtoto akifanya jambo unamwambia. Ni mdogo wetu tutamwelimisha na sidhani kama anamchukia Ommy Dimpoz labda ni maneno tu ya mtaani,” Ali Kiba alisema.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere