Ali Kiba Ampeleka Mzazi Mwenzake Mahakamani Akidai Kudhalilishwa

Staa wa muziki wa Bongo fleva Ali Kiba anadaiwa kumburuza mzazi mwenzake mahakamani na kumtuhumu kwa kumdhalilisha.

Mwezi uliopita habari zilisambaa Kwenye mitandao ya kijamii kuwa Ali Kiba ameburuzwa mahakamani na mzazi mwenzake aliyetambulika kwa jina la Devotha.

download latest music    

Ali Kiba na mwanamke huyo wamezaa mtoto mmoja lakini madai ya mwanadada huyo ni kuwa Kiba alimtelekeza mtoto huyo na kukataa kumpa matunzo baada ya yeye kumchukua kutoka kwa mama yake Ali Kiba alipokuwa anaishi.

Baada ya kuzozana kwa muda mrefu Kwenye mitandao ya kijamii mwanamke huyo alimfungulia kesi Ali Kiba Kwenye mahakama ya watoto Kisutu na mara moja Kiba alitakiwa kufanya DNA.

Lakini sasa inasemekana kuwa Ali Kiba amemfungulia kesi mzazi mwenzake kwenye kituo cha polisi cha Osterbay akidai kuwa amedhalilishwa na mwanamke huyo.

Kiba amesema Kitendo Cha mzazi mwenzake kuongea na vyombo vya habari ni Kitendo Cha kumdhalilisha yeye.

Mzazi mwenzake na Kiba alifanya Interview na Millard Ayo wiki chache zilizopita ambapo alifunguka Mazito Kuhusu Mahusiano Yake na Ali Kiba mpaka kufikia kuzaa naye na sasa kumtelekeza mtoto.

Ali Kiba ameonekana kukasirishwa na mambo yake binafsi ya kifamilia kuanikwa Kwenye mitandao ya kijamii ukitegemea hasa kwa sababu yeye ni mtu mkimya asiyependa kuanika mambo yake Mtandaoni.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.