Ali Kiba Amtaja Ommy Dimpoz Kama Sababu Ya ‘Mo Faya’ Kutoingia Sokoni

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Ali Kiba amefunguk na kuweka wazi sababu iliyosababisha kuchelewa kuingia sokoni kwa kinywaji chake cha Mo Faya.

Ali Kiba alizindua rasmi kinywaji chake Miezi Michache iliuopita kwenye hatusi yake lakini tangu hapo kinywaji hicho hakijaonekana Tena kikiwa kinauzwa sokoni.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Shilawadu ya Clouds Tv, Ali Kiba ameweka wazi kuwa sababu pekee iliyofanya mpaka kinywaji hivho kuchelewa kuongia sokoni ni maradhi ya msanii Ommy Dimpoz ambaye amemtaja kama balozi wa kinywaji hicho.

Mo Faya zilitakiwa ziingia mtaani toka Idd lakini tumepata mtihani kidogo, mtihani tulioupata ni kwamba balozi wetu (Ommy Dimpoz) anaumwa sana, nasikitika kusema hivyo kwa sababu hali yake si nzuri lakini kila siku kunakuwa na uhafadhali, ndio ninachosubiriwa.

Hali yake ikiwa sawa wakati tunazitambulisha anatakiwa awepo. Tunahitaji hali yake iwe sawa, tunatamani awepo”.

Ommy Dimpoz yupo nchini Afrika ya kusini kwa ajili ya kufanyiwa matibabu baada ya kufanyiwa operesheni mwezi uliopita.

Lakini pia Ali Kiba amekana tetesi zilizokuwa zimesambaa kuwa vinywaji hivyo vimepigwa stop na Serikali kutokana na kukosa ubora.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.