Ali Kiba Asajiliwa Rasmi Kuichezea Coastal Union

Staa wa muziki wa Bongo fleva Ali Kiba amekuwa muwazi juu ya mapenzi yake kwa mchezo wa mpira wa miguu na hata kudai kuwa endapo asingekuwa msanii wa muziki basi angekuwa mchezaji wa mpira.

Baada ya Tetesi za muda mrefu hatimaye Uongozi wa klabu ya Coastal Union ya jijini Tanga umethibitisha kutarajia kumsajili msanii wa muziki wa Bongo, Alikiba kwaajili kuitumikia timu hiyo msimu ujao wa ligi kuu soka Tanzania Bara.

download latest music    

Kupitia kipindi cha Esports kinacho ruka kwenye radio ya E FM, Mwenyekiti wa klabu ya Coastal Union, Steven Mguto amethibitisha kuwa kwenye mazungumzo na msanii huyo ili kupata huduma yake ya kukipiga katika kikosi cha wagosi hao wa kaya.

Kiukweli siku zimebaki kidogo lakini na sisis kama zoezi letu limefikia ukingoni nafikiri mpaka kesho tutakuwa kwenye nafasi nzuri ya kueleza nani na nani tumemsajili.

Kwa sababu kwa sasa ndiyo tunamalizia watu wengine maswala ya mikataba sasa sirahisi kuweza kumtaja mkataba bado haja saini mwisho wasiku anaweza akageuza nia na ikawa kitu kingine.

Kwa kiasi kidogo kuna ukweli wa kutaka kumsaini Alikiba lakini pia mambo haya jakaa sana sawa lakini wenyewe mnamuona naye ni mchezaji ingawaje si wa kiwango cha juu kwasababu hana mazoezi ya mara kwa mara ya kucheza mpira hivyo kuwa katika mazungumzo ni kweli“.

Alikiba amvaye anafanya vizuri na wimbo wakeboard wa Mvumo wa Radi huwenda akaanza kuonekana kwenye mechi mbalimbali za ligi kuu kupitia na timu yake ya Coastal Union endapo usajili huo utakamilika.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.