Ali Kiba Ataja Sababu Ya Kufuta Nyimbo Yake

Staa wa Muziki wa Bongo fleva Ali Kiba amefunguka na kutaja sababu za kifua wimbo wake wa ‘Hela’ ambao ulifutwa Kwenye mtandao wa Youtube masaa machache baada ya kurushwa.

Siku ya jana Ali Kiba alikumbana na lawama na kejeli za mashabiki wake mitandaoni baada ya kufuta wimbo wake mpya wa ‘HELA’ aliouachia usiku kupitia mtandao wa YouTube kisha kuufuta asubuhi, amefunguka sababu za kufuta wimbo huo.

download latest music    

Siku yenyewe haikuwa siku yangu ambayo napenda ku-release nyimbo, ilikuwa siku ya Jumanne, so tukamwambia jamaa autoe, inatakiwa siku kama ya leo Alhamisi, ndiyo maana ulikuta umetoka kwenye YouTube, ila sasa hivi ukiingia utaikuta”.

Alikiba amelazimika kutoa maelezo hayo baada ya kushambuliwa na mashabiki kuwa ameutoa wimbo huo kwa kuwa ni mbaya huku wengine wakidai amerudia wimbo wake wa zamani.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.