Ali Kiba Avunja Ukimya Kuhusu Uteuzi wa Jokate

Staa wa muziki wa Bongo fleva Ali Salehe Kiba amevunja ukimya na kufunguka kuhusu uteuzi wa aliyekuwa mpenzi wake Jokate Mwegelo kuwa mkuu wa wilaya ya Kisarawe.

Ali Kiba ambaye alikuwa mpenzi wa Jokate amefunguka Kwenye mahojiano na Millard Ayo Tv,  kusema anamtumia salamu za pongezi na kumtakia kila la Kheri;

download latest music    

Siwezi kulizungumzia sana hilo lakini kwa ufupi tu ni kwamba nimefurahi na nampa hongera sana”.

Lakini pia kaka wa Ali Kiba, Abdu Kiba ambaye pia alikuwa na ukaribu na Jokate amefunguka na kumpongeza Jokate:

Namtakia kila la heri na aweze kuongoza vyema Kwenye uongozi wake. Sijapata nafasi ya kuongea naye kwa sababu naamini yuko bize lakini pia sijawahi kuwasiliana naye kwa kipindi kirefu lakini Kupitia hii Interview namtakia kila la kheri Kwenye maisha yake”.

Jokate aliteuliwa siku chache zilizopita na Raisi John Pombe Magufuli kuwa mkuu wa Wilaya ya Kisarawe.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.