Ali Kiba- Mama Yangu Amenisapoti Kimuziki Kuliko Baba

Staa wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘’Mvumo wa Radi’ Ali Kiba amefunguka na kumtaja mama yake mzazi kama mtu ambaye amekuwa akimsapoti kimuziki Kuliko Baba yake.

Ali Kiba amekuwa akionekana akiwa na ukaribu zaidi na mama yake Kuliko na Baba yake hata Kwenye mitandao ya kijamii amekuwa akionekana akiwa karibu na Mama yake.

download latest music    

Ali Kiba ameweka wazi kuwa Mama yake ndiye mtu aliyemsapoti katika mziki wake tangu anaanza Mpaka sasa tofauti na ilivyokuwa kwa Baba yake Mzee Salehe.

Ali Kiba alifunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na kituo  kimoja cha habari ambapo amefunguka na kusema:

Katika muziki wangu mama yangu ameni support kwa asilimia mia moja tangu naanza Muziki mpaka leo hii”.

Katika jamii zetu za Afrika wazazi wengi wamekuwa wakiamini kuwa muziki au sanaa yoyote ile ni uhuni lakini baadhi ya wasanii kama Ali Kiba wamekuwa wakifuta dhana kutokana na kuwa kioo cha jamii bora na mfano wa kuigwa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.