Ali Kiba na Diamond Uso Kwa Uso Kwenye Msiba Wa Masogange

Staa wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz na hasimu wake namba moja msanii mwenzake Ali Kiba wamekutana Uso Kwa Uso kwenye viwanja vya Leaders Club hapo jana.

Jana Kwenye viwanja vya Leaders Club mwili wa Marehemu Agnes Masogange ulikuwa unapewa heshima ya mwisho kabla ya kwenda  kuzikwa kijijini kwao Mbeya wiki hii.

download latest music    

Wasanii kibao walijitokeza kutoa heshima zao za mwisho na moja wapo walikuwa mahasimu wa siku nyingi Diamond na Ali Kiba ambao walionekana kupeana mkono jambo lililozua minong’ono msibani hapo.

Lakini pia Harmonize alionekana hana tatizo kukaa karibu na Ali Kiba high table wakati misa ya msiba huo inaendelea, hii inaonyesha ni jinsi gani kuna ukweli pale Diamond aliposema WCB haina bifu wala tatizo na Ali Kiba.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.