“Ali Kiba Ndio Anatufundisha Muziki”- King’s Music

Wasanii waliosainiwa chini ya label ya Kings Music ambayo inamilikiwa na staa wa Bongo fleva Ali kiba wamefunguka na kuweka wazi kuwa Msanii huyo ndio anawafundisha muziki.

Kundi hilo la wasanii ambalo linaundwa na wasanii kadhaa Kama Cheed, Killy na K-2GA na akiwemo kaka wa Ali Kiba, Abdu Kiba wamesema Msanii huyo ndio mtu anayewafundisha vitu vingi kuhusu muziki ikiwemo mpangilio wa nani aanze kwenye ngoma zao.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi Planet Bongo ya East Africa Radio, wakati wanatambulisha ngoma yao mpya ‘Toto’, Abdu Kiba  amekiri kuwa kwa ukongwe wa Alikiba kwenye muziki lazima awaongoze.

Anayetupanga ni Alikiba yeye anajua vitu vingi kwenye muziki na ndio maana ana nafasi hiyo ya kushauri nani aanza na nani anafuata na nani atamaliza, kwahiyo Kings Music ni chuo cha muziki”.

Msanii mwingine wa Label hiyo Killy amesema tayari kwa nyimbo mbili ambazo wamezitoa ikiwemo Sina, zimeshawaletea mashabiki wa aina mbalimbali na majina yameanza kuwa makubwa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.