Ali Kiba- Nilivyokutana Tu na Amina Nilijua Nataka Kumuoa

Staa wa muziki wa Bongo fleva Ali Kiba amefunguka kwa mara ya kwanza kukutana na mke wake Bi. Amina Khalef alijua wazi kuwa ndiye mwanamke wa kuoa.

Kwenye Interview Baby kipindi cha Leo Tena cha Clouds Fm, Amina ameweka wazi kuwa yeye na Ali kiba walikutana Kwenye ndege na wakabadilishana namba na kuwa marafiki:

download latest music    

Mara ya kwanza kukutana na  ilikuwa kwenye ndege na hatukuzungumza mara ya pili Kaka yangu binamu ndiyo alinikutanisha nae maana walikuwa marafiki sana na hapo ndiyo tulianza urafiki wetu kabla ya kufika hapa tulipo“.

Hata hivyo, Bi. Aminah amesema kuwa Alikiba ndiye aliyeanza kumtamkia kuwa anampenda na yeye akamwambia kama ni kweli aende kwa wazazi wake akajitambulishe.

Ali Kiba na yeye ameweka wazi kuwa alivyokutana na Bi Amina mara moja akajua yule ndio mke wa kuoa hivyo mara moja akamfuata gavana wa Mombasa Joho akamwambia anataka kuoa.

Yeah Joho ni mtu ambaye aliniongoza sana kwenye maswala ya msingi, kama nilivyokuwaambia kwenye maswala ya dini, mimi na mke wangu tulikutana Nairobi, tukajuana tukaanza kuwasiliana.

Tulivyokuwa marafiki na Hassan nikamwambia kaka kuna msichana anakaa hapa, akaniambia kama ni kuoa basi process zifuatwe nilipoonja Mo Faya tu!, nikaoa hapo hapo,

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.