“Alichofanya Diamond Ni Kuonyesha Hisia Zake”-Fid Q

Image: msanii wa hip-hop,Fid q

Msanii mkongwe , Farid Kumbanda maarufu kama Fid Q ambae yupo kwenye game tangu miaka ya 90 na mpaka sasa amekuwa akifanya vizuri katika game lake la sanaa ya muziki amefunguka na kumtetea Diamond kwa kila alichokifanya katika wimbo wake aliomshirikisha unaojulikana kwa jina la Fresh Remix.

Katika wimbo huo  Fid Q aliamua kumshirkisha Diamond Platinumz katika remix na  diamond aliimba style ya kuchana , kitu kilichoonyesha kwa mashabiki pia kumbe Diamond anaweza kufanya vitu tofauti tofauti katika muziki, hata hivyo pamoja na wimbo huu kutoka  kuna  baadhi ya mashabiki waliupokea vizuri  lakin pia wapo ambao waliongea vibaya kuhusu wimbo huo na kusema Diamond ameimba taarabu.

download latest music    

Katika wimbo huo ambao kuna baadhi ya mashairi ilikuwa kama anamlenga mpinzani wake katika muziki, ukisemekana ulikuwa una lengo la kurusha dongo gizani na kutoa mapovu kwa mshindani wake huyo.Hata hivyo msanii Fid Q  amefunguka na kumtetea Diamond na kusema kuwa sio kweli kuwa wimbo huu diamond amefanya uonekana kama wa taaarabu ila amefanya sahihi kwa sababu ameimba hisia zake.

‘”kwenye hiphop ukishapanhga kufanya collabo  na mtu na mmeshapanga itoke, hata kama kakuchana inabidi tu itoke,kufuta mashairi ya mtu ni makosa‘” aliongea Fid Q katika kipindi cha xxl cha clouds tv alipokuwa akiulizwa alipokeaje baadhi ya komenti za mashabiki wake

Hata hivyo Fid Q bado alisisitiza kuwa, baaadhi ya nyimbo watu uimba kwa hisia hivyo Diamond kuchana maneno yale kwenye wimbo ni swala la yeye kuonyesha hisia zake” bado nasisitiza alichokifanya baba Tiffah katika wimbo wa Fresh remix ni kitu sahihi kwa sababu zile  ni hisia zake,na maisha yake ya kila siku,ni kitu sahihi wala sio taarabu”

Wimbo huo ambao uliachiwa mwezi Agosti mwaka huu ulileta tafrani kwa baadhi ya mashabiki wa upande wa pili na kusababisha marumbano makubwa ya majibizano kati ya ‘team mbili yaan ‘team kiba’ na ‘team diamond’ huku team kiba wakishtumu msanii huyo kuwa ameimba kwa lengo la kutoa mipasho kwao.Hata hivyo original ya wimbo wa Fresh bado unafanya vizuri .

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.