Alichojibu Linah Kwenye Comment ya Hamisa Ni Utata

Instagram sasa imekuwa mtandao usiokuwa na siri , watu wanaotumia mtandao huo wanazidi kuongezeka siku hadi siku, hivyo mambo mengi yanayofanyika yanakuwa yanaonekana kwa watu wengi, mara nyingine unaweza kuhisi hakuna hatakaeona, au watakaona ni wachache kuhusu kile unachoandika au kupost lakini si kweli.

kuna screenshot zinazosambaa katika mtandao wa instagram zikionyesha comments za Hamisa na Linah katika moja ya picha Linah alizopost hivi karibuni akiwa na baba wa mtoto wake,katika posti hiyo ambayo inaonekana kama kama kuna siri chini ya kapeti kuhusu uwepo wa mwanamke mwingine mjamzito mwenye mahusiano ya kimapenzi na mzazi mwenzie na Linah.

download latest music    

Katika post hiyo Hamisa aliandika”lv unajua kuwa kuna mwenzio ana mimba$$$ mdomo koma lakini” maneno haya yanayoonyesha kama kuna kitu Hamisa anajua kuhusu mwanamke huyo mwingine mwenye mimba hivyo inakuwa kama anatoa tarifa kwa Linah.

Lakini kitu cha kushangaza ni jinsi Linah alivyamua kumjibu Hamisa kuhusu taarifa hizo ambapo anaonyesha kujua kwa taarifa hizo na anaonekana kutokujali kuhusu maneno hayo” @ hamisamobetto, Najua, tulishayaongea kuna lingine” alijibu linah

Linah Sanga ambae miezi michache iliyopita alifanikiwa kupata mtoto wa kike mwenye jina TracyParis aliezaa na mpenzi wake  , alisikika hivi karibuni akisema kuwa yeye na mzazi mwenzie huyo wanategemea kufunga ndoa ukiachalia mbali tofauti zao za kidini .

Comment ya Hamisa kwa Linah.

Hata hivyo bado kunakuwa na mishangao kwa baadhi ya watumiaji wa mtandao huu wa kijamii , tena wengine wakimtolea mapovu mwanadada Hamisa mobeto kwa kitendo chake cha kuandika kitu kama hicho ambacho pengine ilipaswa kuwa siri ya familia tu, hii ina maanisha nini kuwa watu hawa wawili wapo katika , je Hamisa alishindwa kuongea na mwanadada Linah nje ya hapo.Je swala hili linapokelewaje na mwanaume aliyehusika katika jambo hili?

Hamisa Mobeto ambae hivi karibuni alikuwa na kashfa nzito ya kuvujisha picha za faragha na msanii mkubwa Tanzania na Duniani kwa ujumla Diamond Platinumz, baada ya msanii huyo kukataa katika vyombo vya habari kuwa mimba na mtoto aliyejifungua Hamisa sio wake , lakini baada ya hapo msanii huyo aliamua kukiri hadharani katika media na kusema kuwa mtoto huyo ni wa kwake.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.