Alichokisema Meneja wa Harmonize Kuhusu Kolabo Ya Diamond na Omarion

Kwa muda mfupi sana kumekuwa na mafanikio yanayoendelea kupishana na kuongezeka kwa msanii Diamond Platinumz ambae anafanya vizuri sana katika kazi zake, Diamond ambae hivi karibuni amefululiza kutoa nyimbo nyingi na  zote zimekuwa zikifanya vizuri sana.Hivi karibuni Diamond alipokea tuzo kutoka Universal  Afrika baada ya wimbo wake wa Marry You  kufikisha views millioni 17 kwenye Vevo akaunti yake, na kupewa tuzo ya heshima iliyojulikana 6x Platnumz Award.

Katika mtandao wa instagram kumesamba picha zilizomuonyesha Diamond akiwa na msanii mwingine mkubwa kutokea bara la Ulaya, Omarion, msanii ambae alishawahi kufanya kazi zake na wasanii wengine wakubwa duniani kama kina Chris Brown. Picha hizo zinaonyesha jwasanii hao wapo katika moja ya location kwa ajili ya nyimbo mpya.

download latest music    

Ricardo Momo ambae ni meneja wa msanii Harmonize ambae pia ni msanii kutoka lebel ya Wasafi ameandika maneno mazuri ya kumpongeza lakini pia kumtia moyo ‘Piga ndinga Simba Tanzania yote inakubali na inatambua mchango wako kwenye muziki usione wanaokutukana kama hawakupendi vile..hapana sasa  jua kuanzia leo hawa watu wanakupenda  kuliko hata tulio karibu yako ila kutokana na hali ngumu ya mjomba Magu wanaona bora watumie njia ya kukupinga japo inauma kumpinga unaempenda ilimradi waongeze followers ili wapige matangazi kwa maana wewe ndie msanii unaeongoza kwa like na comments nyingi kwa yoyote atakaepost .sasa ulitaka wamtusi nani kama sio wewe mtoa ajira mitandaoni..#ABoyFromTandale ” Aliandika Ricardo katika akaunti yake ya instagram

Diamond amekuwa msanii mkubwa na anaeongoza sasa Tanzania kwa kufanya nyimbo na wasanii wengi wa nje, lengo lake ni kutangaza muziki wake na muziki wa Tanzania nje na mipaka ya Afrika.Diamond ni moja ya wasanii waloingia katika game kwa muda  mfupi lakini ameonyesha juhudi na jitihada kubwa ya kitu anachokifanya, anachokifanya Diamond ni zaidi ya kazi lakini pia anapenda kile anachokifanya kwa faidia yake na faida ya Taifa pia.

Kolabo anayoifanya sasa na omarion itakuwa ni moja ya kolabo nyingi anazoendelea kufanya ambapo hivi karibuni tena ilioonekana akifanya na Rick Ross.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.