Alichosema Linah Kuhusu Ku-Copy Wimbo wa Vannesa na Maua

Hivi karibuni wasanii wawili wa kike Linah pamoja na Recho wametoa wimbo wao mpya uliokwenda kwa jinala same boy wimbo ambao inasemekana kuwa umekopiwa kutoka katika wimbo wa Maua na Vannesa mdee uliotoka miezi kadhaa iliyopita.

Hata hivyo moja ya wasanii hao, Linah Sanga amekanusha  tetesi hizo za kuiba idea ya wimbo huo  na kusema kuwa nyimbo hizo ziko tofauti na hata idea zake ziko tofauti wanachowaomba mashabiki kukaa na kuzikiliza vizur na watagundua kitu.

download latest music    

Akiongea katika kipindi cha Playlist cha Efm, Linah anasema kuwa wimbo wao na Recho ulitengenezwa siku nyingi kabla hata wimbo wa Bounce haujatoka lakini walikuwa wamechelewa kuuachia wa sababu ya vitu tofauti tofauti tu.

hii ya kwetu inazungumzi kuwa sisi wote kwa pamoja tunamtaka mwanaume mmoj lakini ile ya kwao inaelezeaa kuwa wao wanatembea na mwanaume mmoja na bado  hawajuani lakini kwa upnde wa ya kwetu ni kwamba tunajuana kuwa tunamtaka mwanaume mmoja.

Wimbo huu wa Linah na Recho unakamilisha nyimbo mbili kwa wasanii hao kufanya pamoja ambapo walifanya wakwanza wakiwa na Makomandoo.

Recho anaanza kurudi kwa kasi sasa baada ya kukaa muda mrefu bila kufanya kazi za muziki kutokana naathari alizokuwa amezipata baada ya matumizi ya madawa ya kulevya.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.