Alichosema Zabibu Kuhusu Shughuli ya Mumewe Uwanjani
Mwanadada zabibu kiba ambae ni dada wa Alikiba na Abdul Kiba amefunguka na kuzungumzia swala la mume wake anapokuwa uwanjani akisakata kabumbu .Zabibu anasemakuwa amefurahi sana kudhuhudia mume wake akicheza uwanjani na kwa jinsi anavyomuona anaamini kuwa atafanikiwa sana.
Zabibu kiba ameyasema hayo baada ya mechi ya ligi kuu nchini afrika kusini ambapo timu yake ya Boroka Fc ilipokuwa ikimenyana uwanjani na timu ya Orlando pirates .
Zabibu anasema kuwa alichokiona kwa mume wake ni nidhamu ya hali ya juu kwa mchezaji huyo kitu mabacho kimekuwa kikileta mafanikio makubwa sana kwa wachezaji wengine na kuwafanya wafike mbali sana katika mpira.
Zabibu pia amefurahi kuwepo Afrika ya Kusini huku akisema kuwa mndhari yake ni tofauti na yale ya tanzania hata viwanja vyake vya mpira viko vizuri kwa mchezaji kujituma kufanya vizuri katika mechi.