Alikiba Alinisaidia Hasimu Wake Diamond Alinitosa- Wastara

Muigizaji wa Bongo movie Wastara Juma au maarufu kama Wastara Sajuki ameibuka na kumlalamikia Diamond kwa kitendo chake cha kukataa kumpa msaada na kudai Alikiba alimsaidia.

Wastara alisafiri wiki chache zilizopita kwenda nchini India alipoenda kupata matibabu kutokana na kusumbuliwa na mguu aliokatwa miaka kadhaa iliyopita baada ya kupata ajali ya gari.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Kikaangoni ya East Africa Tv, Wastara amefunguka na kudai kuwa Ali Kiba alifanya shoo kwa ajili yake ili amchangie Dedham ambazo zilimsaidia katika matibabu yake ya mguu ambapo ni tofauti na alichofanya hasimu wake  Diamond ambaye hakumsaidia chochote.

Niliandika barua ya kuomba msaada, nilimuandikia Diamond lakini watu wake wa karibu walimfikishia taarifa kuwa mimi ni tapeli hivyo hakuweza nisaidia lakini pia wakati huo huo nikamuandikia barua Alikiba na Alikiba aliniambia kuna watu waliokuwa na shoo yao Kenya ila walikuwa hawana fedha yeye wanazozihitaji ila akanihaidi ataenda kufanya shoo ili aje kunisaidia kweli alikwenda na aliporudi aliniletea fedha hizo”.

Lakini stori za mitandaoni zinadai sababu kubwa ya Wastara kupotezewa na Diamond ni yeye mwenyewe kuweka wazi kuwa ni Team Alikiba na sio team Diamond.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.