Aliyekuwa meneja wa Juma Nature aeleza sababu ambazo msanii huyo hafanyi vizuri kwenye muziki kama zamani

Juma Nature ni msanii ambaye amekuwa akifanya muziki kwa muda mrefu sasa. Hata hivyo muziki wake wa hivi sasa unaonekana kutofanya vizuri kama hapo mbeleni.

Meneja wake wa zamani, Mkubwa Fella hata hivyo aliweza kuweka sababu za Juma Nature kufeli hivi karibuni katika interview yake.

download latest music    

Kulingana na Mkubwa Fella, msanii huyu amekosa kampani mzuri ambayo itamuelekeza kufanya muziki ambao unawafurahisha mashabiki wake kama kitambo. Fella alifunguka na kusema
“Juma Nature muziki wake haujapungukiwa chochote, yule kapungukiwa kampani yangu. Kwa sababu alichokuwa anafanya ni kile kile, ila kwa sasa amekosa kampani yangu,” alisema Mkubwa Fella. “Mimi naweza kuongea na mwenye redio vizuri, mimi naweza kuongeza na Dj vizuri. Juma Nature anaimba vizuri pia ni mtunzi mzuri kwahiyo mimi nachoweza kusema kwa Nature ni hilo,”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua