Aliyekuwa meneja wa Young Dee adai kuwa msanii huyu amerudia kutumia madawa ya kulevya

Image: Young Dee

Young Dee amejipata matatani baada ya Max Rioba aliyekuwa meneja wake kupitia label ya MDB kusema kuwa msanii huyu amerudia madawa ya kulevya na kuwa hana bidii kwenye kazi yake tena.

Max alifunguka kusema haya baada ya Young Dee kudai kuwa alimtoroka meneja huyu baada ya kujua kuwa alitoka na mrembo wake, Tunda. Hata hivyo Max amedai kuwa msanii huyu wa bongo amepoteza muelekeo wake kama anaweza kusingizia kuwa alitoka na Tunda ilhali anajua kilichofanya wawili hawa kuacha kufanya kazi pamoja.

download latest music    
Young Dee na aliyekuwa meneja wake, Max

Akizungumza kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM Maz alisema,

“Mimi sikuwahi kumfukuza huyo mtoto kwaajili ya Tunda. “Nimemfukuza sababu ya matumizi yake ya dawa za kulevya na utovu ya nidhamu na ujinga ujinga wake. Kwani mara ngapi Tunda amekuwa na Dee tukiwa naye hapa, yeye Dee kasema ni moja kati ya sababu za kuondoka hapa, sio kweli sina chochote na huyo mtoto,”

Max aliendelea kwa kusema,

“Nachojua ni kwamba ana wakati mgumu sana kwenye game, industry imebadilika, kuna watoto wamekuja wanafanya vizuri, ndio maana anaendelea kusema Dimaond hawezi kushuka kwa sababu anajijua anachofanya, Dee hana heshima na nidhamu kwenye kazi hana.”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua