Amber Lulu Adai Kuwa Akimwagwa na Prezzo Atarudi Kwa Young Dee

Muuza nyago kwenye video au video queen maarufu aliyegeukia Bongo fleva, Amber Lulu amefunguka na kudai kuwa endapo Prezzo atamwaga basi hataona hiyana kurudi kwa Young Dee.

Amber Lulu amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na Prezzo msanii maarufu kutoka Kenya kwa miezi kadhaa sasa lakini imekuwa ikionekana kuwa mpenzi wake wa zamani rapa Young Dee anahusishwa sana au anatajwa sana kwenye mahusiano hayo.

download latest music    

Amber Lulu na Young Dee walikuwa wapenzi kwa kipindi kirefu ambapo kutoka katika vyanzo mbali mbali vilidai kuwa Amber alimpenda sana Young Dee ingawa alikuwa anamfanyia ndivyo sivyo, kuna siku hadi rafiki wa karibu wa Amber Lulu, Gigy Money alisikiaka akisema “Amber Lulu anampenda sana Young Dee sema tu Young D mwenyewe hataki kitulia”.

Hata hivyo hapa kati Young D na Amber Lulu waliingia katika majibizano ya kwenye mitandao ya kijamii baada ya kurushiana maneno mazito ambapo kisa kilianza baada ya  Amber Lulu kumtolea povu mtu alipomlinganisha Prezzo na Young Dee na kudai asimlinganishe mpenzi wake Prezzo na vitu vya ajabu.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Amber Lulu alimtolea povu shabiki wake ambaye alimhoji endapo kuwa tetesi zinazoenea mtandaoni kuwa ameachana na mpenzi wake Prezzo zina ukweli wowote, badala ya Amber luli kumjibu shabiki huyo kama jibu ni ndiyo au hapana badala yake alimtolea povu zito na kuandika “Ndiyo siku nikiachana na Prezzo lazima nitarudiana na Young Dee”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.