Amber Rutty Mpenzi Wake Hoi Gerezani
Msanii Amber Rutty na mpenzi wake ambae wanasota gerezani mpaka sasa kwa kukosa dhamana baada ya kuingizwa selo wakiwa na kosa la kuvujisha video walizojirekodi kinyume na kanuni na hata kuizfanya zikasambaa katika mitandao ya kijamii.
kwa chanzo kinachotoa habari za wawili hao zinasema kuwa wawili hao kwa sasa wameanza kuonekana kudhoofika sana huku sababu kubwa ikihisiwa kuwa wawili hao walikuwa na ugonjwa wa kifua kikuu.
Moja ya ndugu wa karibu wa Amber Rutty anasema kuwa wawili hao walikuwa wakiumwa ugonjwa huo kabla ya matatzio haya kuwakuta na waliwahi kuzidiwa sana hata kusafirishwa kutoa jijini mpaka rifiji ambapo ni nyumbani kwa mwanaumekwa ajili ya kuuguzwa huko.
Hata hivyo baada ya kupata nafuu walirudi mjini kuendelea na shughuli zao, ndugu huyu anasema kuwa hivi karibuni walikwenda kuwaangalia hali zao wakiwa huko gerezani na ndipo walipowakuta wameanza tena kudhofika sana.
Ndugu huyo anasema kuwa wamekuwa wakifanya mchakato kwa ajili ya kupata dhamna ili kunususru hali za ndugu zao.
Baada ya hapo waandishi wa habari walipata kuzngumza na kiongozi mmoja wa kituoni hapo na yeye alisema kuwa hajapata taarifa za ugonjwa wao lakini pia kama kweli ni wagonjwa basi kunataratibu huwa zinafuatwa na kupata matibabu lakini hawezi kutoa taarifza za mgonjwa au mahabusu.