Angalia Alichofanya Diamond na Kuwapita Wasanii Wote Wa Afrika

Mwanamuziki Diamond Platnumz amezidi kudhihirishia watu ustaa wake baada kuzidi kuupeleka muziki wa Bongo fleva mbele zaidi na kupata mafanikio kiasi cha kuvunja rekodi ya Afrika.

Siku ya Ijumaa nchini South Africa Diamond alipewa tuzo na label ya Universal music kwa wimbo wake wa Marry you aliomshirikisha mwanamuziki Neyo kutoka Marekani kuuza vizuri kwa kiwango cha platnum Mara 6 kuwahi kutokea kwa msanii wa Afrika kwa label hiyo.

download latest music    

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Diamond alifunguka yafuatayo kuhusu tuzo hiyo:

Leo nimekuwa msanii wa kwanza wa kiafrika alosainiwa Universal music group co kufikisha mauzo ya nyimbo yake platinum mara sita mfululizo kupitia nyimbo ya marry you  niliomshirikisha Neyo, kwa  niaba ya timu yangu na Neyo tungependa kuwashukuru mashabiki na media zote ulimwenguni”.

Mwishoni mwa wiki hii pia Diamond alionekana akifanya video ya wimbo na mwanamuziki mwingine kutoka Marekani Omarion, ambapo baadae Diamond alithibitisha kuwa amemshirikisha kwenye nyimbo yake mpya.

          Diamond na Omarion              

Kwenye mahojiano aliyoyafanya Mara baada ya kutua Tanzania siku ya Jana, Diamond alifunguka nyimbo hizo alizofanya na wanamuziki kama Rick Ross na Omarion zote zitapatikana keen he album yake mpya itakayoitwa A boy from Tandale ambayo hajataja tarehe rasmi ya kutoka.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.