Angalia Jinsi Nahreel na Aika Walivyotangaza Ujauzito Wa Aika (picha)

Wanamuziki Nahreel na Aika au kwa pamoja maarufu kama ‘Navykenzo’ wameweka wazi ujio wa mtoto wao jana usiku kwa kupitia kurasa zao za Instagram.

Wawili hao ambao  sio tu wanamuziki toka kundi moja la Navykenzo bali pia wamekuwa wapenzi kwa miaka zaidi ya tisa wametangaza kuwa wanatarajia kupata mtoto hivi karibuni ingawa hawajatoa taarifa za zaidi lakini kilichovutia wengi ni staili waliyotumia kutangaza jambo hili la baraka.

download latest music    

Aika na Nahreel waliweka picha ya chumba cha mtoto kwenye nyumba yao wanayopenda kuiita Casadekenzo baada ya muda watu mbalimbali walianza kuwapongeza.

Nahreel aliweka picha hii kwenye ukurasa wake wa Instagram
Aika aliweka picha hii kwenye ukurasa wake wa Instagram

Nahisi wametimiza maneno yao kwani mapema mwaka huu kwenye mahojiano aliyoyafanya na East Africa tv, waliweka wazi wanategemea kuhamia kwenye jumba lao la kifahari walilo jenga lakini pia wanataka mtoto maana nyumba ni kubwa sana.

NavyKenzo ni kundi la mziki wa kizazi kipya ambao wametamba na vibao vyao kama ‘game’ ‘kamatia chini’ na hivi sasa wanafanya vizuri na wimbo wao wa ‘bajaji’.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.