Asha Baraka Awajia Juu Wasanii Wenye Asili Ya Kongo

Mkurugenzi wa African Stars Entertainment (ASET), Asha Baraka amegeuka mwiba mkali kwa kuwachamba wanamuziki Raia wa DR Congo wanaofanya shughuli ya muziki nchini kwa tabia zao za kutohudhuria misiba ya wanamuziki wenzao wasio raia wa nchi yao.

Asha Baraka aliwachamba raia hao waliofurika Ukumbi wa Vijana uliopo Kinondoni jijini Dar, Jumatano iliyopita kwenye msiba wa mwenzao, Erick Cantona ‘Mugogo wa Mazizini Msanii wa Bei Kali’ aliyefariki Jumamosi iliyopita kwa ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar.

download latest music    

Mkurugenzi huyo aliwatolea mfano wa kifo cha mwanamuziki na kiongozi wa Bendi ya Vijana Jazz, Abdallah Mgonahazeru ambaye msiba huo walifurika wanamuziki na wasanii wa filamu lakini hakukuwa na mkongomani hata mmoja.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.