Aslay aeleza kwanini hawezi kubali kusainiwa Wasafi

Dogo Aslay ambaye yuko katika lebo ya Mkubwa na Wanawe amefunguka na kusema kuwa hawezi kubali kujiunga na lebo ya Diamond Platnumz – Wasafi.

Staa huyo wa Yamoto Band ambaye ameanza kutoa nyimbo zake binafsi amesema kuwa malengo yake yamezidi kuwa msanii wa Wasafi ya Diamond.

download latest music    
Aslay

Aslay alieleza kuwa mipango yake ni kufikia kiwango cha Diamond na Ali Kiba kwa hivyo hawezi kusainiwa na Wasafi kama anataka kufikia malengo yake.

“Kusainiwa WCB hapana, kwa sababu mimi nina ndoto za kuwa zaidi ya WCB au kuwa zaidi ya kitu kingine chochote, naamini nitakaza nitafika hizo sehemu, naweza kusema nina ndoto za kufika kama alipofika Chibu, nina ndoto za kufika kama alipofika Ali Kiba. Inabidi nikaze niwe mimi kama mimi nitafute njia ya kutoboa nifike level hiyo, yaani sio yeye pekee yake mtu yeyote, wakisema wanisaini siwezi kukubali sasa hivi”  Aslay alisema katika kipindi cha XXL ya Clouds FM.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere