Aslay Akiri Kuumia Moyo Baada Ya Kumwagana na Mama Watoto Wake

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Aslay Isihaka amefunguka na kuweka wazi kuwa Kitendo Cha kuachana na kama watoto wake bado kinamuumiza mpaka leo.

Miezi michache iliyopita Aslay alikiri kuachana Rasmi na aliyekuwa na mpenzi wake kwa muda mrefu Tessy Chocolate ambaye pia amezaa naye mtoto mmoja.

download latest music    

Kwenye mahojiano na gazeti la Mwanaspoti, Aslay ameweka wazi kuwa hapendelei sana kuongelea kuachana kwake na Tessy lakini hawapo pamoja:

Huwa sipendi kulizungumzia hili suala kwa sababu linaniumiza sana, ila ukweli ndio huo kama ulivyosikia nimeachana na mama Moza.

Ni mambo ya familia na kilichobaki kwa sasa ni uhusiano wa wazazi wenye mtoto, ambaye anahitaji uangalizi wa pande zote. Unajua kuna baadhi ya watu wanadhani kuwa hii ni kiki, lakini mimi sio mtu wa kiki kabisa na ninazungumza hapa ni ukweli mtupu”.

Aslay amedaiwa kuwa Kwenye Mahusiano na Muigizaji wa Bongo movie Diana KImario na pia Tessy ametajwa kuwa Kwenye Mahusiano na mwanaume mwingine ambaye ni Kigogo fulani mjini.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.