Aslay Anatarajia Kumpa Kolabo Diamond

Mwanamuziki anayefanya vizuri na wimbo wake wa ‘natamba’ Aslay amesema anatarajia kumpa kolabo msanii mkubwa wa bongo fleva, Diamond Platnumz.

Aslay anayesifika kwa kutoa nyimbo mara kwa mara na sio bora tu nyimbo bali nyimbo zinazopendwa na mashabiki zake amesema kuwa anategemea kuachia nyimbo yake mpya hivi karibuni.

download latest music    

Mtayarishaji wa muziki hapa nchini, Shirko ambaye pia ndiye aliyeandaa nyimbo mbili za Aslay ambazo ni ‘natamba’ pamoja na ‘natamba’ amesema kuna uwezekano Mkubwa ambao wanatazamia kufanya ‘remix’ ya ngoma hiyo ambayo tayari inafanya vizuri ya ‘natamba’ na msanii pekee wanayemwangalia ili ashirikiane na Aslay kwenye wimbo huo si mwingine bali ni Diamond.

Diamond ambaye tayari na yeye anahit na wimbo wake wa ‘halelujah’ uliovunja rekodi na Kuwait msanii wa kwanza Tanzania kufikisha waangaliaji milioni moja kwenye mtandao wa Youtube ndani ya masaa kumi na tano. Pia na Diamond alishawahi kusema Kuwait angependezwa zaidi kama angepata nafasi ya kufanya kazi na Aslay kwaiyo bila Shaka utakuwa wakati mzuri kabisa kuwapa mashabiki zao kile kitu wanataka.

Aslay amezidi kufanya vizuri zaidi kwenye mtandao wa youtube kwani kwenye wiki ya kwanza video ya wimbo huo kutoka alimtoa Diamond kutoka kwenye namba moja na kuishikilia kwa wiki kadhaa mpaka alipokuja kutolewa juzi na msanii kutoka wasafi Harmonize na wimbo wake wa ‘shululu’.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.