Aslay apagawisha jukwaa la fiesta Arusha,nyimbo zake zote zaimbwa.

Ikiwa imepita siku moja tu tangu tamasha la fiesta lizinduliwe rasmi tarehe 9 septemba ,mkoani Arusha ambapo tamasha ilo hujumuisha wasanii wengi wakubwa na wachanga  nchi Tanzania na hata nje ya nchi,msanii kutoka Tanzania aliyekulia kwenye muziki tangu akiwa na umri mdogo ameacha historia ya kuliteka na kulitawala jukwaa .Msanii huyo ambae kwa sasa anatamba na kibao chake kipya cha “pusha”.

Aslay  hivi karibuni amefululiza kutoa nyimbo nyingi,na licha wa upya wa nyimbo izo bado mashabiki wake walionekana kuimba nyimbo zote tena bila kumpa nafasi msanii huyo kuiba na kipaza sauti,mashabiki walionekana kuwa na mzuka wa kila nyimbo alikuwa anaianzisha kitu kilichamfanya Aslay kushindwa kabisa kuimba muda mrefu,lakini hii ni dalili tosha kuwa msanii Aslay amekuwa akikubalika na kufatiliwa na mashabiki wake kwa ukaribu sana.Aslay alisikika akiwaambia mashabiki zake kuimba hadi kiitikio huku mashabiki wakionekana kuwa na shangwe la kutoka katika kila wimbo aliimba hadi wimbo mpya uliotoka hivi juzijuzi wa pusha.

download latest music    

Hata hivyo kwa hivi karibuni Aslay ameonekana kulitawa vizuri jukwaa na kupokea shangwe za kutosha kutoka kwa mashabiki wake akiwa jukwaani mfano mzuri ni katika tamasha la hivi karibuni la  usajili wa  tigo fiesta na show ndogo iliyoandaliwa mkoani Mtwara na kituo cha television cha clouds Tv show  inayojulikana kama ‘jiwe la mwezi’  yenye lengo la kutoa zawadi kwa msanii alifanya vizuri kwa mwezi huo,huku mashabiki wakionekana kumpa sapoti kubwa alipokuwa jukwaani.

Hongera kwake bwana Aslay tunaamini mafanikio haya yataendelea kwa show zote za fiesta zijazo na matamasha mengine pia.keep it up!

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.