Aslay avutwa kwenye mgogoro baina ya Diamond na Ali Kiba

Aslay sasa ni miongoni mwa wasanii ambao wamejipata pabaya kwa kuonekana kujihusisha na Ali Kiba.

Msanii huyo wa Yamoto Band alisemekana kuwa eti atatoa wimbo na Kiba hivi karibuni, madai ambayo yanaonekana kuwa uvumi tu.

download latest music    

Meneja wa Aslay, Chambuso, amemtetea msanii wake huyo kuwa hajawahi kuwa na ukaribu wowote na Ali Kiba.

Akiongea katika kipindi cha FNL, Chambuso amesema hakuwa na wimbo wowote ambao Aslay ameurekodi na Ali Kiba kama inavyosemwa na baadhi ya watu.

Chambuso pia aliogezea kuwa hakuna tatizo lolote kati ya Aslay na kundi la WCB.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere