Aslay Kumsaidia Enock Bella Kimuziki Kwa Kolabo

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Aslay Isihaka amefunguka na kuweka wazi kuwa ana mpango wa kumshika mkono na kumsaidia Msanii mwenzake kutoka Yamoto Band Enock Bella.

Aslay alikuwa mmoja wa wasanii waliounda kundi la Yamoto Band lakini baada ya kundi hilo kuvunjika miaka michache iliyopita kila msanii alishika njia yake.

download latest music    

Baada ya kila msanii kuendelea na kazi zake binafsi Aslay alionekana kupata mafanikio makubwa zaidi lakini pamoja na Beka Flavor ambaye pia amekuwa anafanya vyema na Mbosso aliyesainiwa WCB amekuwa anafanya vizuri pia.

Lakini Enock Bella aliyekuwa maarufu kwa kuimba bezi kwenye Yamoto amekuwa akisuasua tofauti kabisa na wenzake kwani ameshatoa nyimbo kadhaa ambazo hazijafanya vizuri kabisa.

Kwenye mahojiano na kipindi cha Kikaangoni cha EATV, Aslay amefunguka na kukiri kuwa kuna jitihada anafanya kwa ajili ya kumsaidia msanii mwenzake Ikiwa ni pamoja na kolabo hivi karibuni:

Ndio Enock Bella yupo na ninaongea naye na pia Bado Yupo Kwenye grupu moja kwaiyo bado tuna ukaribu na kuna jitihada tunafanya kwaiyo inshallah siku is nyingi mashabiki wataona kitu kutoka kwetu ingawa siwezi nikakiongelea sana”.

Enock Bella alitangaza kusainiwa kwenye label iliyopo nchini Uganda mwaka jana mwishoni lakini baada ya muda mfupi akatangaza kujitoa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.