Aunty Ezekiel Amwaga Povu Baada Ya Tuhuma Za Kurudia Nguo

Muigizaji wa filamu za Bongo Movie na mfanyabiashara Aunty Ezekiel ameibuka na kumwaga povu kwa watu waliokuwa wanamsema amerudia nguo aliyovaa Kwenye msiba wa mtoto Patrick.

Siku ya Jumamosi Aunty Ezekiel aliungana na Familia ya Muna na ndugu jamaa na hata wasanii wenzake katika mazishi ya Mtu Patrick yaliyofanyila katika viwanja vya Leaders na kuzikwa Makaburi ya Kinondoni.

download latest music    

Lakini mara tu baada ya kupigwa picha akiwa amevaa gauni lake jeusi  mjadala mzito uliibuka Kwenye mitandao ya kijamii ambapo watu walimtuhumu kwa kurudia nguo ile aliyokuwa amevaa Kwenye msiba.

Baada ya kuona mjadala huo mtandaoni Aunty alitumia ukurasa wake wa Instagram kumwaga povu ambapo aliwataka watu wasimfatilie kuhusu mavazi yake na ni uamuzi wake kurudia nguo kwani hakuna anayejua maisha yake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Aunty Ezekiel aliandika:

Naomba niseme hivi mimi huwa sifanyi maisha ya maigizo 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.