Aunty Ezekiel: Sioni Tatizo Kuvaa Nguo Niliyoshonewa na Mobetto

Muigizaji wa Bongo movie Aunty Ezekiel amewatolea povu zito watu wote waliomkoso kwa kuvaa nguo aliyoshonewa na Mwanamitindo Hamisa Mobetto.

Siku ya uzinduzi wa filamu yake fupi ya Mama Aunty alivaa nguo nzuri nyekundu na kupendeza kupita kiasi ambapo baadae aliweka wazi kuwa aliyemshonea nguo ile ni Hamisa.

download latest music    

Mashabiki wengi walimjia juu Aunty kwa kuvaa nguo ya Hamisa huku akijua wazi yule ni adui namba moja wa Zari na pia adui wa shoga yake Wema Sepetu.

Kwenye mahojiano na gazeti la  Amani, Aunty amekiri kutowaelewa wanaoshangaa ishu hiyo kwa sababu yeye na Mobeto hawana ugomvi wowote na wala hajawahi kukosana naye, sasa kitakachomfanya ashindwe kuvaa nguo aliyomshonea ni kitu gani?.

Mimi ninawashangaa sana wanaoongea kuhusiana na kuvaa nguo ambayo nimeshonewa na Hamisa. Sioni tatizo kwani tofauti zake na mtu mwingine mimi hazinihusu“.

Mashabiki ambao ni Team Zari wamekuwa wakimtolea maneno Aunty kwa usaliti aliofanya kwa Zari kwani wengi waliamini kuwa ni rafiki yake lakini kama utakumbuka siku za nyuma Aunty alishasema kuwa hana urafiki na Zari wala Hamisa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.