Aunty Ezekiel- Zari na Hamisa Sio Marafiki Zangu

Muigizaji wa Bongo movie Aunty Ezekiel amefunguka na kuweka wazi kuwa hana urafiki wowote na Mama watoto wa Staa Diamond, Zari na Hamisa Mobetto.

Kwa muda mrefu inajulikana kuwa Aunty Ezekiel ana urafiki na Wema Sepetu kwaiyo siku ambayo alionekana na Diamond na Zari visiwani Zanzibar wakila bata watu wengi walichukulia kama usaliti kwa rafiki yake.

download latest music    

Hivi sasa Tetesi zinadai kuwa Diamond yupo Kwenye Mahusiano na Hamisa Mobetto ambaye ni adui namba moja wa Wema Sepetu hivyo Kolabo mtu amekuwa akihoji Aunty atakuwa upande gani kama ni Hamisa au Wema?.

Lakini Aunty ameshaweka wazi kuhusu hilo na kudai hahitaji kuchagua upande kwa kuwa Zari na Hamisa sio marafiki zake bali Wema ndiye rafiki yake.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Dizzim Online, Aunty ameweka wazi kuwa Diamond sio bosi wake bali ni mshkaji wake wa siku nyingi kabla hata hajaanza Mahusiano na Moses Iyobo.

Naseeb is not my boss, Naseeb mimi ni rafiki yangu na mshkaji wangu ni mtu ambaye nimejuana naye kabla ya kujuana na hawa watu wengine wote yaani tumejuana kivyetu na sio Kupitia Mahusiano yetu.

Hamisa sio rafiki yangu na wala Zari sio rafiki yangu na hata mwanamke mwingine wa Diamond sio rafiki yangu lakini Wema mimi ni rafiki yangu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.