Aunty Lulu Atoa Ofa Kwa Papii Kocha.

Mwanadada aliyewahi kujipatia umaarufu wake kwa kazi ya utangazaji ambae pia haachi kuwa na drama za mara kwa mara, Aunty Lulu amefunguka na kusema kuwa yupo tayari kumpa ofa msanii wa muziki papii kocha kwa muda wot mpaka asahau maisha ya jela aliyoyapitia.

Aunty Lulu anasema kuwa amemuona papii kocha na ameona jinsi ambavyo amekuwa akipendeza na kuwa mpya hivyo yuo tayari kumpa penzi litakalomfanyua asahau shida na mateso aliyokuwa ameyapitia kipindi yupo jela.

download latest music    

Aunty Lulu ambae amejisifia kuwa anajua sana kupenda amesema kuwa yuko tayari endapo msanii huyo atakubali kumpatia nafasi.

Unajua mimi najua kupenda,endapo nitampatia penzi papii kocha mbona atasahau kabisa alipotoka.Yeye akubali tu mbona sijawahi kuona mahusiano yake,naamini kwa kipindi alichokaa jela kama angekuwa na mwanamke angekuwa tayari ameshajitokeza siku nyingi.-Alifunguka Aunty Lulu.

Jitihada za kumtafuta papii kocha ziligonga mwamba baada ya simu ya msanii huyo kutokupatikana ili kujulishwa taarifa hizo.

Papii kocha na baba yake walikuwa wasanii wa muziki waliofanya vizuri kwa muda mrefu lakini kazi zao zilisimama baada ya kukaa jela kwa muda mrefu kwa kosa la kulawiti watoto , lakini mwaka 2017 mwishoni wasanii hao walipokea msamaha wa rais na kuachiwa huru.

wasanii hao sasa hivi wamepanga kurudi kwa kasi ya ajabu huku wakiwa chini ya studio ya Wanene Entertainment huku wakipokea msaada na uangalizi wa wizara ya habari na michezo ili waweze kuimarika kimuziki.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.