AY na MwanaFA tayari kulipwa bilioni 2.1 baada ya kushinda kesi dhidi ya Tigo

Kampuni ya mawasiliano ya Tigo imepata pigo baada ya mahakama kutupilia mbali rufaa waliokata katika kesi yao dhidi ya wanamuziki AY na MwanaFA.

Mwaka jana mahakama Wilaya ya Ilala ilikua iliamuru kampuni hio kuwafidia AY na MwanaFA bilioni 2.1 kwa kutumia nyimbo zao bila kuwalipa.

download latest music    
AY na MwanaFA

Tigo ilikata rufaa katika mahakama kuu ya Tanzania kupinga agizo la mahakama wilaya ya Ilala iliyowaagiza walipe AY na MwanaFA bilioni 2.1.

“Ni haki yao kulipwa kwa sababu ni kazi zao ambazo zinalindwa kisheria,” Albert Msando, wakili wa wasanii hao wawili, alisema baada ya uamuzi huo wa koti.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere