Baada ya Diamond Platnumz kuzindua perfume yake, King Kiba kuingiza bidhaa moto moto sokoni

Image: Alikiba

Japo King Kiba amekuwa kimya kwa muda sasa msanii huyo amefunguka na kusema kuwa sasa hivi anajiandaa kuachia bidhaa kadhaa kutoka kwa AK na sasa King Kiba.

Ali Kiba

download latest music    

Kwa sasa muimbaji huyo wa Aje ameachia shati na kofia ambazo zimekuwa zikiuzwa Afrika Mashariki. Lakini kwa sasa anatarajia kuachia viatu, glasses na energy drink. Alisema haya kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM.

“AK ni brand ya Alikiba nashukuru imekuwa kubwa watu wanavaa lakini pia ipo na ya King Kiba nayo ni brand yangu na zipo official kabisa na kazi zitakapoanza watapata product zote.”

Aliongeza kwa kusema kuwa anamalengo makubwa na ndio maana bidhaa zake zinachukua muda kuachiliwa sokoni.

“Kuna malengo makubwa sana tumeyaweka lakini siwezi kusema sasa hivi ila kuna jeans, viatu na glasses tayari zishatoka soon wataziona maana hizi zitakuwa za kwanza sababu tayari zishatoka na kuna energy drink”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua