Baada Ya Kolabo na Sauti Sol, Tegemea Kolabo Ya Alikiba na Kundi Jingine Kutoka Kenya

Staa wa muziki wa Bongo fleva aliyeendelea kufanya vizuri na ngoma yake ya ‘Mvumo wa radi’ Ali Kiba amedaiwa kuwa yupo njiani kuachia Kolabo yake mpya na kundi la H-art kutoka Kenya.

Bongo 5 wanaripoti kuwa Alikiba ameingia tena studio wikiendi hii nchini Kenya akiwa na kundi la H-Art The Band kuandaa mdundo mpya.

download latest music    
Ali Kiba akiwa na The H-Art Band

Inadaiwa kuwa ngoma hiyo itakuwa ni ya Alikiba akiwa amewashirikisha H-Art The Band na tayari wiki hii wameshamaliza ku-shoot video ya wimbo huo.

Alikiba toka wiki iliyopita yupo nchini Kenya kwa kazi hiyo maalumu ya kuandaa ngoma hiyo na imeandaliwa na producer maarufu nchini Kenya, Cedo.

Kama utakumbuka mara ya mwisho Ali Kiba ametoa wimbo na kundi la muziki kutoka Kenya Sauti Sol wimbo uliotwa ‘Unconditionally Bae’ ulikuwa bonge la hit hivyo tutegemee mambo mazuri kutoka kwa King Kiba.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.