Baada Ya Kupewa Kichapo na Mama Diamond, Hamisa Afunguka

Muigizaji wa Bongo movie na mfanyabiashara Hamisa Mobetto amefungukia skendo ambayo imekuwa ikimzunguka kwa siku kadhaa sasa ile ya kupewa kichapo na Mama Diamond.

Kuna habari zilisambaa siku chache zilizopita ambazo zilikuwa zinadai kuwa Mama Diamond alimpa kipigo cha mbwa koko Hamisa baada ya kumkuta nyumbani kwa Diamond Madale.

download latest music    

Mama Diamond alithibitisha taarifa hizo Baada kuwaambia Global Publishers kuwa hampendi Hamisa na kila atakapokutana naye basi atampiga tena kwa kudai amekosa adabu na hataki mtoto wake awe naye.

Kwenye mahojiano na waandishi wa habari, Hamisa alikataa kuliongelea  jambo hilo na kudai ni  binafsi zaidi ila kugombana kwa binadamu ni kitu cha kawaida.

Hilo siwezi kuliongelea, yeah!. is too person, is too private, is too family. Hata vikombe kwenye kabati vinagong’ana, so sisi binadamu vinaweza kutokea”.

Lakini pia Hamisa aliulizwa nini Mahusiano Yake na Mama Diamond ambaye yeye alisema kabisa kuwa hampendi, alifunguka;

Sina kinyongo na mtu, sina bifu na mtu, mimi am just fine, may be yeye mwenyewe sio upande wangu wa kuweza kuelezea”.

Sakata hilo linasemekana kuleta sintofahamu kati ya Diamond na mama yake kwani kwa hivi sasa Diamond yupo Kwenye Mahusiano na Hamisa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.