Baada Ya Kuzikosa Pesa Za Diamond, Hamisa Mobetto Kaja Na Hili

Mwanamitindo Hamisa Mobetto amefunguka mara baada ya habari kusambaa kuwa mahakama imetupilia mbali madai yake, ametangaza kuja na duka lake la kuuza nguo.

Mara baada ya kujifungua mtoto wa Diamond miezi mitatu iliyopita, Hamisa na Diamond waliingia katika mgogoro ambao ulipelekea Diamond kukataa kutoa pesa kwa ajili ya kumuhudumia mtoto kitu kilichomsukuma Hamisa kutafuta wakili wa kumwakilisha na kuenda kumfungulia kesi ya madai Diamond Mahakamani Kisutu.

download latest music    

Siku ya Ijumaa, tarehe kumi kesi hiyo ilitupiliwa mbali na hakimu mkazi Kisutu kwa kile kilichodaiwa kuwa ni makosa katika hati ya awali ya mashtaka ambapo wakili wa Mobetto, Good luck Walter alidai kuwa karani wao alikosea kuchapa hati hiyo ikiwa ni kosa la kibinadamu kabisa.

Kwa kipindi kirefu mashabiki wamekuwa wakimtupia vijembe Hamisa kuwa ni mwanamke asiyetaka kujishughulisha kuwa hana kitu hana biashara yoyote zaidi ya kutegemea matunzo kutoka kwa baba za watoto wake Majizzo na Diamond.

Lakini mapema wiki hii kupitia ukurasa wake wa instagram tayari Hamisa amefunguka na kudai kuwa Ana mpango wa kufungua duka lake hilo la nguo na pia amekataa tuhuma alizokuwa anarushiwa kuwa amejibweteka tu kwani tayari ana biashara zake tangu siku nyingi ambazo watu wengi hawazijui.

 Instead of being rich at once it is better to be poor first, kwa takribani miaka minne sasa nimekuwa nikifanya biashara ya kuuza nguo (kitu ambacho watu wengi hawakijui) Imekuwa ndio biashata inayonilisha na kunitunza mimi na familia yangu, nilikuwa napiga picha naweka nguo zangu kwa baadhi yq maduka yenye majina makubwa hapa mjini wananiuzia na ninapata pesa kwa njia hiyo, watu wengine walikuwa wananidhihaki sana kwa kusema oh ananipa picha tu ndio anachojua bila kujua kinachoendelea. Ata ourclosettz ilikuwa mali yangu lakini hakuna anayejua. Sasa habari njema nimeaua kufungua duka langu mwenyewe litakaloitwa Mobettostyles naomba support yenu tafadhali”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.